KITENDA WILI"NYUMBA YANGU NDOGO LAKINI INAENEA WATU WENGI' MBUTA NANGA!!

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO TZUK

FLORA LYIMO BLOG

FLORA LYIMO BLOG

FLORA

FLORA

FLORA NA RAIS JK

FLORA NA RAIS JK

FLORA NA MH PINDA

FLORA NA MH PINDA

SHINY ,HEALTHY-LOOKING AND GORGEOUS HAIR' WHATSAPP +44 778 7471024

SHINY ,HEALTHY-LOOKING AND GORGEOUS HAIR' WHATSAPP +44 778 7471024

Friday 30 September 2011

DDC Mlimani Park - Uzuri wa Mtu Sio Sura*-*WIMBO PIA WATUFUNDISHA KITU HUU" SIKIZA KWA MAKINI" KUTOKA -YOU BEEN SNAP* AIBU ,AIBU ,NA MASIKITIKO KWA BAADHI YA WATANZANIA MLIOPO UGAIBUNI .HASA HAPA ULAYA -LONDON NILIPO NA NINAPOYAONA KWA MACHO. WACHAFUAJI WA SHUGHULI ZA WATU HASA KWENYE HARUSI'S"



SALAM WATANZANIA WENZANGU, POPOTE PALE MLIPO HASA LONDON!

MAMBO YA KUJIREKEBISHA .NA NIMEONA NIWAAMBIE MAANA ASIE WAAMBIA NDO ASOTAKA MAENDELEO NA SIFA ZA WATANZANIA*

KWANZA KABISA. *KWENYE HARUSI*
Hivi mbona mnaalikwa kwenye Harusi nyingi alafu mnafika kuzichafua? yani tunashindwa na wenzetu kule Tanzania tena walokuwepo mashambani , yani mtu unaalikwa na unaambiwa RANGI ZA HARUSI hiyo na unaamua kujivalia utakacho wewe na siyo atakacho yeye au wao wenye harusi hizo , kwa mfano wengine mnajitolea kuvaa sare na kusimamia harusi hizo ,huku mnaenda kujinunulia nguo zenu za kwenda vilabu usiku kwa shughuli zene, bila KUJALI KWENYE HARUSI HIZO .KUNA WATU WAMAANA ,KUNA BABA'S, MAMA'S ,KAKA'S ,BIBI'S BABU'S NA SIJASEMA WATOTO , maana wengi maarusi hawawaruhusu watoto ..kwa sababu zao wazijuazo wenyewe. sasa basi chakushangaza ni kwamba , mbona msinunue vitambaa vya bei powa yani hata vitenge vya maana huku ulaya ni £5. chakumtosha mtu nguo yake ya heshima kabisa ,ya kiharusi ? kweli mwatia aibu ,kama huwezi kununua nguo ya harusi hiyo bora hata usifike maana ,unamchafulia mwenzio ON HER ONLY BIG DAY FOR HER LIFE... na wengi siyo kwamba hamna hizo nguo, au uwezo wakuzinunua ..mnazo na sababu yakusema hivyo ni pale unamuona mtu kaenda kununua hako ka nguo cha kuendea club usiku na kajisahau kwamba anaenda harusini..ALAFU yeye ndo yupo mstari wa mbele kukazania kupiga picha na maharusi hao ,huku mpaka sidiria na matiti yapo nje ,nje..na utaona yupo kwenye karibia picha zote za harusi hiyo ..yani wewe jiulize ,je ,utakuja kumuonyeshaje mwanao picha hizo na huwezi kujikata kwenye picha hizo maana yeye ndo kachukua karibia nafasi nzima ya picha hizo.au yupo katikati ya picha hizo.
Na hasa huku Ulaya wanzungu au wenzetu wa makabila mengine wanaposikia harusi ya WATANZANIA hufika au kuzisubiria picha na kutaka kuona je ni vipi WATANZANIA wanavyozisherekea harusi zao na wanavaa vipi ? alafu wewe NENDA  chungulia picha nyingi za harusi humo facebook ujionee vituko ..na wengi mna WEKA MAKOMMENTS umependeza kulikoni ,umependeza sana, sasa hapo chacha"..na huku unajua wazi hajapendeza na bora asingelikuwepo hapo kabisa.Mbuta Nanga! CHA MUHIMU CHA KUFANYA WEWE USIWEKE COMMENT ,WACHA BILA COMMENT MWENYEWE ATAJUA NI KWANINI UMEZIRUKA ZOTEEEEE..UKAACHA HIYO ...kama umemuogopa kumuambia..ila ni kibinadam hatuambiani ukweli ..maana unapomuambia mtu ukweli ndo basi unatafuta uadui..ILA MIMI SIPO KWA KUJALI UADUI ..NAKUAMBIA UKWELI UKICHUKIA NA KUUKARIBISHA UADUI HUO NI JUU YAKO NA UAMUZI NI WAKO.ila utajirekebisha lini kama hujaambiwa? WATANZANIA HASA UK.tujfunze maendeleo ,upendo na ukweli ,SAINI YA UTANZANIA WETU na yeyote anayetaka maendeleo. NAONA WENGINE MNAJIULIZA NI KWANINI NIKASEMA WALOKUWEPO UK, nimesema hivyo maana ndipo ninapoishi na kujionea vituko hivyo kwenye mashughuli ya watu hasa maharusini na kuyashuhudia kwa macho..angalieni harusi nyingi huko nyumbani tena migombani zinavyopendeza.. watu wanapeleka mazawadi.Kuna zawadi za aina nyingi na za bei powa hata kadi yatosha ..ili kujitoa aibu hizo..hahahhaa.nimekumbuka nilikuwepo kwenye harusi moja, sasa watu wakaambiwa ni wakati wakuzitolea zawadi zenu kwa maharusi ,watu wamebakia kuangaliane, mie nikajiandaa na kazawadi kangu ,alokuwa ka kaa pembeni na mimi akaniambia, MIMI ZAWADI YANGU ILIKUWA KUBWA SANA SIKUWEZA KUILETA" je utamfikiria vipi Mdau ? .mie nikabakia kucheka nikamuuliza kwani ulimnunulia gari au lile kabati la baridi.? ( fridge ) na kama ndo hivyo basi ungelikuja na kadi iloandikwa hivi "zawadi yako njoo chukua mahali fulani ,kwani sikuweza kuileta kwa ukubwa wake".huo ndo ustaarabu " au mwaonaje , jamani si hivyo ni vihoja harusini "
ANYWAY .nihayo tu kwa leo maana nimeshindwa kuvumilia kwa kuona HARUSI NYINGI ZINAVYOCHAFULIWA NA PIA ZINATIA AIBU KUZIWEKA PECHA NA KUSEMA HARUSI YA FULANI ILOFANYIKIA ,LONDON , MAREKANI .NK.. na lingine nimesahau .. HIVI KWANI NI LAZIMA MTU UFUNGE HARUSI HUKU UKIWA MJAMZITO!MIMBA KUBWA MPAKA NGUO ZINAKUKATAA" ...yani KAMA SIYO UONEVU ..WENGI MNAFAHAM UJAUZITO ULIVYO NA MAMBO YAKE..mmeo mtarajiwa na wengine wote wanaifurahia harusi hiyo basi wewe hujiwezi kwa kila kitu kwako ni kichefu chefu ..na upende usipende ni lazima uchovu kuwanao mpaka hata hutamaniki ..kama wabisha wewe bisheni ILA CAMERA ISHATANGAZA YOTE.. ok ..wengine mtasema mmepata mimba hizo njiani mwa ndoa hizo .basi na vile vile za weza kuairishwa mpaka pale utakapo zaa..yani ili nyote kuzifurahia harusi hizo ..ILA ISIWE TABU ,MAANA WENGINE UNAWEZA KUWA MNANDOTO ZENU ZA MWISHO WA DUNIA..NA KUTAKA KUZIFUNGA NDOA HIZO FASTA..KUYESHE ,KUCHOMOZE JUA..PAKA AU MBWA KUFARIKI"
CHA KUJIREKEBISHA NI ..MAVAAZI YA KWENYE HARUSI ..NA NDO MAANA WAZUNGU WASHATUAMBIA (DRESS CODE).wale wengi wenu mnajivunia kuwa wamujini ..tena ndo wakwanza kuharibu na huku mnavyojiringishia hum kwenye FACEBOOK kuwa mmesoma mpaka sijui matawi gani "..sasa dress code mbana za washinda ngudu zangu" jua HARUSI NI HUHIM KWA WANAOZIFUNGA NA HESHIMA NI VIZURI KUKUWEPO NA UNAPOAMUA KUJITOLEA KWA CHOCHOTE NI BORA NAWE UYAHESHIMU MANENO YAO...KAMA HUJAPATA HIYO DRESS CODE.BASI VAA NGUO YA KUJIHESHIM,NAKUWAPA HESHIMA WALE WAKUBWA WALOKUWEPO"

 "SASA NIMEKUAMBIA NA NIMEWAAMBIENI UKWELI .JIREKEBISHENI, TUPENDANENI NA KUTAKIA TANZANIA YETU ,AMANI ,UPENDO NA UMOJA.
GOD BLESS YOU ,GOD BLESS DUNIA IWE PAHALI PEMA PAKUISHI NA KUYAMALIZIA MAISHA YETU AMENI"
Awapendae na kwaambia Ukweli
"MISS FB -FLORA BAHATI LYIMO"

No comments:

Post a Comment